Picha: Kubadili dhana ya Afrika kupitia sanaa
Maonyesho ya sanaa katika makavazi
ya Guggenheim mjini Bilbao, kaskazini mwa Uhispania, inalenga kuonyesha
kizazi kipya cha Waafrika ambao wanalipa bara hili mtazamo mpya.
Maonyesho hayo kwa jina Making Africa yanashirikisha wasanii 120.
Mmoja
wa wale ambao kazi zao zinaonyeshwa ni mpiga picha kutoka Senegal Omar
Victor Diop. Kazi zake huangazia kuonyesha mchanganyiko wa tamaduni
nyingi nchini humo. Hufanya kazi na wahusika, kama huyu Mame-Diarra
Niang kwenye picha ambayo Diop aliipiga kuonyesha sifa mbalimbali za
watu.kizazi kipya cha vijana mji mkuu Maputo. Kando na kuonyesha usasa, picha zake pia hujaribu kuonyesha studio zilivyokuwa zamani.
Mkenya Cyrus Kabiru naye hutengeneza vitu mbalimbali kutoka kwa vitu vilivyotupwa kama taka. Ametengeneza vitu vingi sana vya kuvaliwa, kwa mfano miwani hii, ambayo inadhamiria kuonyesha jinsi Afrika kutazamwa visivyo.
Bodys Isek Kingelez naye dhamira yake kuu ilikuwa kuonyesha majengo ya siku za usoni na kukosoa mtazamo wa miji ya Kimagharibi.
Muundo huu wake, aliouita Congolese Red Star, pia unaashiria maadili ya kijamaa na msanii huyu anasema anataka kuunga ulimwengu wenye miji iliyojaa "amani, haki na uhuru".
Raia wa Nigeria JD Okhai Ojeikere naye ameangazia jinsi wanawake husuka nywele zao. Alitaka kuweka kumbukumbu ya mitindo yote ya kusuka nywele pamoja na kuwafanya watu wengi zaidi kuikumbatia.
.
Maonyesho hayo ya sanaa ambayo kwa Kiingereza yanaitwa Making Africa yataendelea mjini Bilbao hadi Februari 21.
No comments:
Post a Comment